Hatari kubwa kwa watoto
Watoto wachanga na wakubwa huwa hatarini kubwa ya kuathiriwa na silaha za nyuklia.
Ni rahisi kwao kufa kutokana na majeraha ya kuchomeka wakilinganishwa na watu wazima (kwani ngozi zao ni nyembamba na nyepesi), majeraha kutokana na milipuko (ikitiliwa maanani udhaifu wa miili yao) na ugonjwa uletwao na mnururisho mkali (kwani wana chembe nyingi za uhai zinazokua na kugawanyika kasi).
Kadhalika, huwa sio rahisi wao kujinusuru kutoka kwa majengo yaliyobomoka na kuchomeka au kuchukua hatua nyingine kufuatia mlipuko kwa lengo la kuongeza nafasi zao za kuponea na kuendelea kuishi.
