Silaha hatari zaidi ulimwenguni
Silaha za nyuklia ndizo haribifu zaidi, zisizobagua na za kinyama zilizowahi kuundwa. Bomu moja lina nguvu tosha za kuharibu jiji nzima na kusababisha maafa ya makumi ya maelfu, iwapo sio mamilioni ya watu.
Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu limezitaja silaha za nyuklia kuwa na “nguvu haribifu za kipekee kwa mateso yasiyo na kifani zinazosababisha … na ni tisho kwa mazingira, vizazi vijavyo na hasa maisha ya binadamu”.
Silaha hizo hutoa kiasi kikubwa cha mnururisho, huchafua hewa, ardhi, maji na miili yetu na kusababisha madhara yanayoenea kutoka taifa moja hadi jingine na vizazi hadi vingine.
Ilimradi silaha hizo zipo, pana hatari kubwa kuwa zitatumika tena, na matokeo yake yatakuwa maangamizi, ikiwa ni pamoja na kwa watu wa mataifa yasiyohusika na mapigano ambapo zinatumika.
