SHARE

Dada wawili wa Hiroshima

Kimino Wataoka aliyekuwa na umri wa miaka miwili, na dadake Hirono aliyekuwa na miaka mitano, walikuwa nyumbani na wazazi wao wakati Hiroshima iliposhambuliwa. Wote wanne waliuawa.

Dada yao mwingine, Kayoko, aliyekuwa karibu na kitovu cha mlipuko, alikufa pia. Ni dadao mkubwa pekee, Chizuko, ambaye alinusurika.

Yaaminika picha hii ya Kimino (kushoto) na Hirono (kulia) ilipigwa siku moja kabla ya shambulio la bomu ya nyuklia. Picha na: Miho Iwata