SHARE

Baiskeli ya magurudumu matatu ya Shinichi

Hiroshima ikishambuliwa, Shinichi Tetsutani aliyekuwa na umri wa miaka mitatu alikuwa nje ya nyumba yao akifanya alichokifurahia zaidi – kuendesha baiskeli yake ya magurudumu matatu.

Alipata majeraha makubwa ikiwa ni pamoja na kuchomeka mwili wote, na aliaga dunia saa chache baadaye. Dada zake wawili, Michiko na Yoko, waliuawa pia.

Miaka mingi baadaye, baba yao alisema: “Hili halifai tena kuwatendekea watoto. Tafadhali fanyeni juhudi za kuleta amani duniani na kujenga mahala pa watoto kuchezea mpaka nyoyo zao ziridhike.”

Baiskeli ya magurudumu matatu ya Shinichi iliyochomeka imehifadhiwa katika Jumba la Makumbusho la Hiroshima Peace Memorial, na mchongo wake unapatikana katika Jumba la Makumbusho la International Red Cross na Red Crescent Museum jijini Geneva.

Imekuwa ni ishara inayotia uchungu ya mateso waliyoyapata watoto kwenye mashambulizi ya mabomu ya nyuklia.

Picha na: Jumba la Makumbusho la Hiroshima Peace Memorial Museum, lililotolewa na Nobuo Tetsutani.