Wasiwasi kuhusu ueneaji
Kukataa kwa nchi zenye silaha za nyuklia kupunguza na hatimaye kumaliza zana hizo kumeimarisha hatari ya mataifa zaidi, na hata wahusika ambao si serikali, kupata silaha za nyuklia siku moja. Kupiga hatua katika upunguzaji wa silaha hizo ni hali muhimu ya kuzuia kuenea kwake.
Ingawa hatua muhimu zimechukuliwa kuzuia ueneaji wa silaha hizo, hakuna uhakika kwamba zitaleta matokeo yanayotakiwa. Taifa lolote lenye uwezo wa urani au kutayarisha upya mafuta ya nyuklia ili kutoa plutoni linaweza, kwa kudhania tu, kuunda silaha ya nyuklia ndani ya miezi kadhaa.
Afrika Kusini, Israeli, India, Pakistan na Korea Kaskini zilijipatia silaha za nyuklia kwa kutumia vifaa na nyenzo zilizodaiwa kulenga amani, na hivyo kukariri hatari za kuendelea kuongezwa kwa silaha hizo chini ya mipango ya nguvu za nyuklia.
Kilo kadhaa za urani iliyostawishwa au kemikali ya plutoni zinatosha kuunda bomu moja la nyuklia. Hivi leo, mamia ya tani za nyenzo hizo zimewekwa akiba ulimwenguni, na nyingine nyingi bado zinaundwa. Ni lazima tatizo hilo lishughulikiwe Ili kufanikisha upunguzaji wa silaha hizo za vita.