Majira ya baridi kali ya nyuklia na njaa
Silaha za nyuklia ndizo zana za pekee zilizowahi kuundwa zenye uwezo wa kuharibu aina zote za uhai na hali nyingine za maisha zisizoelezeka kwa urahisi duniani.
Silaha mia moja au zaidi zikitumia kushambulia miji mikubwa, masizi na moshi kutoka kwa mawimbi ya moto zinaweza kuweka pazia la kufunika dunia yote na kuzuia miale ya jua kwa zaidi ya mwongo mmoja, hivyo basi kusababisha kushuka kwa halijoto duniani – athari ijulikanayo kama majira ya baridi kali ya nyuklia.
Ikiwa imetumbukizwa katika giza totoro, dunia inaweza kufikia kiwango cha kuganda, hata katika mazingira ya joto. Mimea ya chakula itaangamizwa na kilimo duniani kuporomoka, na kusababisha njaa kubwa na kuvunjika kwa jamii.
Majanga ya maradhi ya kuambukizana na ugomvi kuhusu rasilmali haba zitaenea. Watu wanaokabiliwa na utapia mlo watakuwa hatarini kubwa ya kufa.
Hata inayojulikana kama vita ndogo ya silaha za nyuklia – ikihusisha sehemu ndogo tu ya silaha za nyuklia duniani – inaweza kusababishia watu duniani hatari ya kufa njaa.
Vita kama hiyo inaweza kudhoofisha ozoni, isababishe ongezeko kubwa la aina fulani za kansa na kuangamiza viumbe na mimea wa baharini na majini. Aina nyingi za mimea na wanyama zitakabiliwa na tisho la kufa na ulimwengu utapatwa na uharibifu usioweza kugeuzika.