Kukwamisha shughuli za ufadhili
Utumiaji wa hata silaha moja ya nyuklia popote ulimwenguni unaweza kutatiza huduma za afya na muundo msingi wake, na hivyo kukwamisha shughuli za ufadhili.
Hospitali na watoaji wa dawa, vifaa vya kuzima moto, mifumo ya mawasiliano na usafiri itabaki kuwa vifusi kote katika sehemu za umbali wa kilomita kadhaa zilizoharibiwa kabisa.
Wanaothubutu kujaribu kuwasaidia wagonjwa na majeruhi huhatarisha maisha yao kutokana na kiasi kikubwa cha unururifu.
Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu limekuwa likionya kila mara kuwa hakuna uwezo kamili wa kuendeleza shughuli za ufadhili na kutoa misaada hitajika silaha moja ya nyuklia ikitumika kufanya shambulizi, na hakuna uwezekano wa kuwahi kuujenga mfumo kamili wa ufadhili na misaada hitajika.
Kadhalika, Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO), limefikia uamuzi kuwa: “Huduma za matibabu zilizosalia haziwezi kupunguza ukali au uzito wa maafa kutokana na silaha za nyuklia kwa njia yoyote ya maana.”
