SHARE

Kutetea marufuku

Ili kulinda wanadamu kutokana na maangamizi na madhara yasiyogeuzika ya silaha za nyuklia, serikali hazina budi kuchukua hatua za dharura ili kumaliza zana hizo.


Makumi ya maelfu ya silaha za nyuklia yameharibiwa katika kuitikia miito ya watu kutoka kote duniani wakihimiza upigaji marufuku wa silaha hizo. Afrika Kusini ndiyo nchi pekee ambayo imemaliza kabisa silaha za nyuklia; nchi nyingine dazeni kadhaa zimetupilia mbali mipango ya kujipatia silaha hizo.

Vita ya maneno na propaganda kati ya nchi za Magharibi na Mashariki ikiwa kileleni, kulikuwa na silaha takribani 70,000 za nyuklia. Upunguzaji mkubwa wa silaha hizo duniani ulitokea katikati ya miaka ya 1980 na mapema 2000.

Lakini katika siku za karibuni, miradi ya kupunguza mabomu ya nyuklia imekwama, huku baadhi ya mataifa yenye silaha za nyuklia yakiongeza hifadhi yake kwa kasi ya kipekee. Hakuna hata mojawapo ya mataifa hayo limetangaza mpango wa kumaliza silaha hizo kabisa.

Hata hivyo, mataifa mengi ya ulimwengu yanapinga vikali silaha za nyuklia na yanataka zimalizwe mara moja.

Haitoshi kukomesha ueneaji wa silaha hizo katika mataifa zaidi, ama kuweka masharti kuhusu hali ambapo zinafaa kutumiwa. Ikitiliwa maanani kuwa silaha hizo ni hatari kubwa kwa maisha yote katika dunia yetu, suluhisho la pekee ni kuzipiga marufuku.

Hifadhi ya Wasanii wanopinga Mabomu. Picha na: Miki Anagrius