SHARE

Kazakhstan: Msanii aliyezaliwa bila mikono

Karipbek Kuyukov alikulia kijijini Yegyndybulak, karibu na Semipalatinsk, Kazakhstan – eneo kubwa zaidi la Urusi la majaribio ya silaha za nyuklia. Anakumbuka akiwa mtoto vile fanicha, vyungu, vikombe na sahani zilitetemeka kila mara mlipuko wa jaribio la bomu la nyuklia ukitokea.

Kabla hajazaliwa, wazazi wake walizoea kwenda juu ya kilima cha karibu na nyumbani kwao ili kujionea vizuri wingu kubwa angavu lenye umbo sawa na uyoga likipaa juu angani.

“Hawakujua kuhusu hatari zilizokabili afya zao na athari angamizi za jinai waliyokuwa wakifanyiwa,” akakumbuka.

Karipbek alizaliwa 1968 bila mikono. Lakini hilo halikumzuia kuibuika kuwa msanii msifika anayetumia miguu yake na mdomo kuchora kwa rangi. Ujumbe mkuu wa kazi zake za sanaa ni kupinga utumiaji wa silaha za nyuklia.

“Kazi yangu maalumu katika ardhi hii ni kufanya kila niwezalo kwa watu walio kama mimi kuwa wahanga wa mwisho wa majaribio ya silaha za nyuklia,” akasema. “Sitaki majaribio hayo yafanyike tena popote au wakati wowote, na kokote katika dunia hii … Anga na ibaki ikiwa safi na watoto wetu wawe na afya nzuri!”

Kuanzia 1949 hadi 1989, Urusi ilifanya majaribio zaidi ya 450 ya mabomu ya nyuklia katika Semipalatinsk, karibu robo ya majaribio yote yaliyofanyika ulimwenguni.

One of ​​Karipbek Kuyukov’s artworks, titled “Fear”.