Kumulikwa na miale ya bomu
Toru Ikemoto alikuwa na umri wa miaka saba, na dadake alikuwa na miaka tisa wakati Hiroshima ilipoangamizwa. Wote wawili walikuwa ndani ya nyumba yao, umbali wa karibu kilomita moja kutoka kwa kitovu cha mlipuko.
Ndani ya siku nne au tano baada ya shambulizi, nywele zao zilianza kung’oka, wakapatwa na homa na kuvuja damu kwenye ufizi – ishara za kuwa na sumu ya mnururisho mkali.
Ingawa wote wawili waliponea madhara hatari ya mwanzo mwanzo ya magonjwa, hatimaye waliaga dunia kutokana na athari za baadaye za mnururisho. Toru alikufa akiwa na umri wa miaka 11 naye Aiko akiwa na miaka 29.
