Tahakiki ya jinsia
Mara nyingi viongozi ambao hutangaza kuwa tayari kutumia silaha za nyuklia hupongezwa wakitajwa kuwa wanaume dume, hodari na wenye uwezo wa kuamua. Kwa upande mwingine, wanaounga mkono kupunguzwa na hatimaye kumalizwa kabisa kwa silaha hizo hupuuziliwa mbali wakitajwa kuwa na tabia za kike, wadhaifu na wenye kuongozwa na mhemuko.
Isitoshe, mijadala ya umma na maamuzi kuhusu silaha za nyuklia mara nyingi hutawaliwa na wanaume.
Kwa kupigana kikamilifu na dhana hizo na kuhakikisha ushirikishwaji zaidi wa jinsia zote, pana uwezekano mkubwa wa kufanikiwa kwa harakati za kupunguza na hatimaye kumaliza silaha za nyuklia.