Kulazimisha watu kuhama na kuporomoka kwa uchumi
Kwenye vita ya nyuklia, mamilioni ya watu wakifikiwa na cheche za mnururisho zinazotokana na mlipuko wa bomu watalazimika kuhamia nchi jirani wakitafuta makao ya dharura, chakula na maji yasiyo na sumu, pamoja na huduma za matibabu. Idadi ya watu wanaotafuta makao nje ya makwao inaweza kuwa kiasi kikubwa ambacho hakijawahi kushuhudiwa.
Utumiaji wa silaha aina nyingi za nyuklia unaweza kuvuruga biashara ya kimataifa na mawasiliano ya simu, redio au televisheni, intaneti na mitandao ya jamii, na pengine kusababisha kuporomoka kwa uchumi duniani, na hivyo kuzorotesha umaskini na kurudisha nyuma malengo ya maendeleo ya binadamu kwa miongo mingi.
Hakuna taifa wala mtu yeyote binafsi awezaye kujikinga na athari za silaha za nyuklia.