“Ilikuwa ni hatua ya kipekee kuanza kuutekeleza Mkataba wa Kupiga Marufuku Silaha za Nyuklia mnamo Januari, 2021, na hatimaye kuelekea kumalizwa kabisa kwa silaha za nyuklia.”
– António Guterres, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, 2021
Kadiri mataifa zaidi yanavyojiunga na TPNW muda unavyoendelea, ndivyo kanuni na matakwa yake zitaimarika, na kuzidisha shinikizo kwa mataifa yenye silaha za nyuklia kukubali kanuni zake. Kufikia sasa, zaidi ya nusu ya mataifa ya ulimwenguni yamejiunga na mkataba huo.
Mkataba wa TPNW unatoa fursa yenye nguvu kwa ulimwengu kuchagua njia mbadala ya kuepuka kubaki ukitawaliwa na vitisho vya maangamizi makubwa ya nyuklia. Unatoa nafasi ya kuendelea mbele wakati ambapo tumefikia upeo wa hali ya wasiwasi mkubwa unaotia hofu.
