SHARE

Hatua zifaazo kuchukuliwa kumaliza silaha za nyuklia

Binadamu ndio waliojenga silaha za nyuklia kwa mikono yao na ni wao pekee wanaoweza kuzibomoa kwa mikono hiyo hiyo. Hapana pingamizi zozote za kiufundi, na zilizopo ni za kisiasa pekee. Makumi ya maelfu ya silaha za nyuklia yamebomolewa.


Maendeleo zaidi katika kupunguza na hatimaye kumaliza silaha za nyuklia yanaweza kupatikana pakiwa na uongozi ulio tayari kuleta matokeo yanayotarajiwa na nia njema ya kisiasa. Ukweli kwamba maeneo makubwa ya ulimwengu yametangazwa kuwa hayana silaha zozote za nyuklia ni kidokezo huenda ulimwengu wote ukawa huru kutokana na silaha hizo.

Baadhi ya mielekeo mipya katika ushindani wa kihistoria wa kumiliki na kusimamia silaha za nyuklia ilipatikana wakati wa upeo wa migogoro ya kimataifa. Hali ya wasiwasi mkubwa inaweza kushawishi fikra za viongozi na kuwalazimisha kutafuta njia mpya za kuendelea mbele.

Lakini mafanikio hutegemea iwapo pana ufuasi mkubwa mashinani unaotetea mabadiliko na kushirikisha raia wahusika wa tabaka zote. Mwiko wa kimataifa ulio thabiti na wa kudumu dhidi ya silaha za nyuklia unatokana na juhudi za miongo mingi za kupinga silaha hizo.

Watu binafsi wanazo njia nyingi za kutumia kuchangia harakati za kumaliza silaha mbaya zaidi duniani. Zifuatazo ni baadhi yake:

Waandamaji waliobeba mienge wapitia jijini Oslo, Norway, wakiunga mkono TPNW. Picha na: Kristian Laemmle-Ruff